Manchester united yakamilisha usajili wa beki kutokea Benfica victor Lindelof mwenye miaka 22.
Kinda huyu kutokea Benfica ameenda kwa ada pauni million 30.7
Manchester united yakamilisha usajili wa beki kutokea Benfica victor Lindelof mwenye miaka 22.
Kinda huyu kutokea Benfica ameenda kwa ada pauni million 30.7
27, apr 2017 ligi ya England alimahalufu kama Premier league iliendelea baadhi ya timu zilicheza katikati ya wiki hii moja. kati ya mechi kubwa ikiyotazamwa na mashabiki wengi wa soka ni kati ya dabi ya jiji la Manchester kati ya man city akiwa nyumbani Etihad Stadium akimkaribisha Man United.
Mpaka dakika ya 90 za mchezo Man city na Man United walitoshana nguvu ya bila kufungana 0-0.
ila kuna matukio mawili yaliyojitokeza ndani ya mchezo huo.
›Tukio la kwanza, mchezaji wa Man united Fellaini kuzawadiwa kadi nyekundu dakika ya 84'.
›Tukio la pili, kipa wa Man city Bravo kupata majelaha katika dakika ya 78' na kutolewa nje kwa matubabu zaidi.
Man city akibaki kwenye nafasi yake ileile ya nne akiwa na point 65 huku akifatiwa na Man United kwa tofauti ya point moja.
Apr 23, 2017 Mbio za kumalizia ligi nchini Spain alimahalufu La Liga jumapili hii kulikua kuna mechi nne ila mechi iliyokua ikatazamwa na wapenzi wa soka duniani ni El Clasico kati ya Real Madrid akiwa nyumbani Santiago Bernabéu akiwakaribisha watani wao wa jadi Barcelona.
Madrid apokea kichapo cha goli 3-2 magoli ya Madrid yakifungwa na Casemiro dakika ya 28 pia dakika ya 77 Sergio Ramos amepigwa kadi nyekundu goli la pili likifugwa na James Rodriguez dakika ya 86.
Magoli ya Barcelona yamefungwa na Lionel Messi dakika ya 33, goli la pili likifungwa na Ivan Raktic dakika ya 73, Lionel Messi kumaliza mchezo dakika ya 90.
Barcelona wanaongoza ligi kwa point 75 sawa na Madrid kwa tofauti ya magoli pia Madrid wapo nyuma kwa mchezo mmoja.
March 4, 2017 ligi kuu ya England baadhi ya mechi zimechezwa siku hii ya leo mechi ya mapema ni kati ya Manchester United akiwa nyumbani Old Trafford akiwakaribisha Afc Bournemouth.
Man United walitegemea mechi hii kuingia top 5 ya ligi kuu ya England ila mambo yamebadilika kwa kulazimishwa suluhu ya 1-1.
Goli la Man United limefungwa na Marcos Rojo dakika ya 23 wakati Zlatan Ibrahimovic kukosa mkwaju wa penati dakika ya 72. huku Bournemouth wakisawazisha goli kwa mkwaju wa penati kupitia kwa mchezaji wao Joshua King dakika ya 43.
Manchester United wamebaki nafasi ya sita kwa jumla ya point 49.
February 26, 2017 ndio siku ya historia kwa kocha wa Man United Jose Mourinho baada ya kuchukua kikombe cha EFL Cup.
Mechi ya fainali iliyochezwa katika uwanja wa Webley ili zikutaniasha timu mbili bola Manchester United na Southampton.
Man United imeibuka washindi wa goli 3-2 magoli yote mawili ya Southampton yakifungwa na Manolo Gabbiadini katika dakika ya 45 na 49. Na magoli ya Manchester United yakifungwa na Zlatan Ibrahimovic dakika ya 19 na dakika ya 87 huku Jesse Lingard akiifungia Man United goli la pili dakika ya 39.
Manchester United imechukua ELF Cup mala 5 huku Zlatan Ibrahimovic ndio amekua mfungaji bola wa ashindano hayo 2017 baada ya kuifungia Man United magoli 4.
Leo February 26 , 2017 La Liga imeendelea kutimua vumbi katika viwanja tofauti tofauti ila wapenzi wengi wa soka walitupia macho kwenye mechi ya Barcelona na Atletico Madrid.
Japo Barcelona imeonesha kiwango kidogo baada ya mechi iliyopata kupoteza zidi ya PSG lakini imeonesha ubola wake leo hii baada ya kupata ushindi mnono zidi ya wapinzani wao wa jadi Atletico Madrid.
Atletico Madrid akiwa nyumbani kwake Vicente Carderon akiwakalibisha Barcelona amepokea kichapo cha bao 2-1.
Magoli ya Barcelona yamefungwa na Rafinha dakika ya 64, wakati dakika ya 70 Diego Godlin akisawazisha , Lionel Messi akimaliza mchezo kwa kuifungia Barcelona goli la pili na la ushindi katika dakika 86.
Barcelona wameka juu jumla ya point 54 wakifatiwa na Real Madrid akiwa na point 52 akiwa anakipolo kimoja mkononi.
25, February 2017 kulikua na mchezo wa maludiano kati ya watani wa jadi Simba na Yanga Ligi kuu Tanzania bara katika uwanja wa Taifa Dar es salaam.
Baada ya sare katika mchezo wa round ya kwanza ya 1-1. Round ya pili imechezwa hii leo na simba kuibuka washindi wa goli 2-1.
Goli la Yanga limefugwa na Simon msuva dakika ya 4 kwa mkwaju wa penati , magoli ya Simba yamefungwa na Laudit Mavugo dakika ya 66, goli la pili lilifugwa na Shiza Kichuya akitokea bechi.
Baada ya mechi hiyo Simba wamebakia kileleni kwa jumla ya point 54 huko Yanga wamebaki na point zake zilezile 49 akiwa na kiporo kimoja.
Usiku wa kuamkia leo umechezwa mechi mmoja kataka kombe la La Liga kati ya Valencia akiwa nyumbani katika uwanja wa Mestalla akiwakaribisha Real Madrid.
Mchezo umemalizika kwa Real Madrid kupokea kichapo kutoka kwa Valencia cha bao 2-1 magoli ya Valencia yakifungwa na Simone Zaza katika dakika ya 5, na dakika ya 9 Fabiani Orellana akiwapatia Valencia goli la ushindi. Goli la kufutia machozi kwa Madrid lilikifungwa na Cristiano Ronaldo katika dakika ya 44.
Real Madrid akisalia nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa ligi akimzidi mpinzani wake Barcelona point moja lakini Barcelona akiwa mbele kwa mchezo mmoja.
Usiku wa kuamkia leo 22 Feb 2017 zilipigwa mechi ya maludiano kombe la UEFA Europa League baadhi ya mechi hizo moja ya mchezo ni kati ya Saint- Etienne akiwa nyumbani akiwakaribisha Manchester united.
Man united baada ya kuifunga Saint-Etienne 3-0 katika mchezo wa kwanza hapo Old Trafford.
Leo hii Saint- Etienne akubali kichapo akiwa nyumbani kwao katika uwanja wa Stade Geoffroy-Gichard Ufarasa kutoka kwa mashetani hao kushinda bao 1-0 goli likifungwa na Hernik Mkhitaryan dakika ya 16. St. Etienne achomolewa kwa jumla ya magoli 4-0 na man united kufuzu hatua ya kumi na sita bola ya Europa League.
Lakini katika mechezo huo yame ambatana matukio matatu tukio la kwa ni mchezaji aliyeipatia goli man united kuingia majeluhi, tukio la pili beki wa man united Eric bailly kupigwa kadi nyekundu katika dakika ya 63 na tukio la tatu kipa wa Manchester united Sergio Romero ni siki yake ya kuzaliwa.
![]() |
PSG VS BARCELONA |
![]() |
Countinho |
Mchezaji wa Manchester united Wayne Rooney ambaye ameitumikia klabu hiyo tangu mwaka 2014 kwa kipindi chote amefanikiwa kuifungia magoli 250 moja kati ya magoli mulwa aliyefunga zidi ya Stoke City January 21, idadi ya magoli hayo yamemfanya kuendeleza ubabe wake zidi ya mchezaji wa zamani wa Manchester united Bobby Charlton mwenye magoli 249.
Mchezo wa mwisho wa kundi A uliochezwa usiku wa January 22, ambao uliwakutanisha mwenyeji wa mashindano hayo Gabon aliyetoa sale na Cameroon mchezo huo ulimfanya Gabon kuaga mashindano hayo baada ya kutoa sale michezo yake mitatu na kumfanya kushika nafasi ya tatu akiwa na point Tatu huku akiambatana na Guinea Bissau aliye shikilia nafasi ya mwisho. Burkinafaso na Cameroon ndio wamewaza kufuzu atua ya robo fainali kwenye kundi A
January 15, 2017 ligi ya England zilipigwa mechi mbili ambazo zilitazamiwa na mashabiki wengi wa soka la ulaya moja kati ya hiyo mechi ni kati ya Manchester united akiwa nyumbani Old Trafford akimkalibisha mtani wake Liverpool mechi ikimalizika kwa suluhu ya 1-1 goli la Liverpool lilifungwa na kwa mkwaju wa penati katika dakika ya na dakik ya Zlatan akiisawazishia united ila goli hilo lilimsisimua mchezaji wa zamani wa Manchester United Rio Fredinand
January 15, 2017 baadhi ya mechi za La Liga ziliendelea moja kati ya mechi iliyoangaliwa na wengi ni kati ya Sevilla akiwa nyumbani akimkalibisha Real Madrid.
Kipindi cha kwanza kilitoka suluhu bila kufungana lakini kwenye dakika ya 67 Madrid walipata mkwaju wa penati kupitia mshambuliaji wao Cristian Ronardo. Magoli ya Sevilla yakifungwa na Sergio Ramos akijifunga kwenye dakika ya 85 na dakika ya 90 Jovetic akiwapatia goli la pili Sevilla
January 15, 2017 zilipigwa mechi mbili ambazo zilitazamiwa na mashabiki wengi wa soka la ulaya ni kati ya Manchester city akiwa ugenini kwa Everton.. Magoli ya Everton yalifungwa na Lukaku dakika ya 34',dakika ya 47 millaras akiwapatia goli la pili ,dakika ya 79 Davies akifunga goli la tatu, dakika ya 90 Lookman akimaliza mchezo kwa city kulala bao nne bila
Usiku wa kuamkia jana mashindano ya Copa del Rey ambopo mechi nne zilichezwa ambazo ni
Alves 1-1 Deportivo
Cordoba 1-2 Alcorcon
Villarreal 1-1 R. Sociedad
Lakini mechi iliyotazamwa na mashabiki wengi ni kati ya Barcelona akimkalibisha Athletic amboyo ilimazimika kwa Barcelona kupata ushindi mnono wa goli 3-1 magoli ya Barcelona yakifungwa na L. Suarez dakika ya 34 , dakika ya 48 Neymar akifunga kwa mkwaju wa penati , na dakika 78 free kick ya Lionel Messi. Ila goli la Athletic club lilifungwa na saborit dakika ya 51 michezo ukimalizika kwa MSN kuifikisha timu yao hatua ya robo fainali.
Mashindano ya AFRICA CUP OF NATION (AFCON) yametalajiwa kuanza hivi punde masani wa Tanzania Diamond platnumz ambaye atakwenda kuburudisha katika ufunguzi wa mashindano hayo hapo January 14, 2017 nchini Garbon Diamond platnumz ameangwa kwa kupewa bendela ya Taifa na waziri wa michezo Nape
Usiku wa January 10, 2017 ilisubuliwa mechi ya wapinzani wa jadi katika kombe la mapinduzi baada ya Azam FC kutinga fainali kwa kushinda bao 1 bila zidi ya Taifa Jang'ombe. Nusu fainali ya pili ilipigwa mishale ya saa mbili katika saa za Afrika mashariki katika uwanja wa Amaan Zanzibar. Yanga na Simba dakika 90 zilimalizika bila kufungana, hivyo ililazimika kupigwa penati ambazo zilimwezesha Simba kufuzu hatua ya fainali kwa penati 4-2 na kukutana na Azam FC January 13, 2017
Mbadala wa aliyekua kocha wa Azam FC kutokea Hispania Zeneb Hernandez, umepatikana hii leo baada ya kumsainisha kocha mpya kwa mkataba wa miezi sita Aristica Cioaba raia wa Romania mwenye umri wa miaka 45. Azam wameingia mkataba na kocha huyo leo huko katika visiwa vya Zanzibar na anategemea kuwepo kwenye mechi yao ya nusu fainali hapo badae kati ya Taifa Jang'ombe.
Shilikisho la soka duniani FIFA january 9,2017 lilitoa tuzo huko mjini Zurich Uswiss, watu wengi walitolea jicho tuzo ya mchezaji bora wa dunia iliyokua ikishindaniwa na Lionel Messi, Cristiano Ronaldo, na Antoine Griezmann.
Ila mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa dunia FIFA alikua ni Cristiano Ronaldo.
January 7, 2017 mchezo wa mwisho kundi B ulichezwa katika uwanja wa Amaan Zanzibar. Azam fc iliyoonekana unasuasua katika mashindano hayo ila usiku huo wa jana Azam ilimshushia kichapo kikali Yanga cha goli 4-0 magori ya Azam FC yalifugwa na John Bocco dakika ya 2, Yahaya mohamed dakika ya 54, na dakika ya 80 Joseph muhundi, na goli la mwisho alifunga Enock Atta. Ushindi huo unamweka Azam FC nafasi ya kwanza akifatiwa na Yanga wakati zimamoto pamoja na Jamhuri wakiaga mashindano
FA Cup yaanza usiku kuamkia leo ilipigwa mechi kati ya westhum wakiwakalibisha Manchester city katika uwanja wa London stadium. Westhum wapokea kipigo chini ya kocha pep Guardiola cha 5 bila magoli ya man city yakifugwa na Yaya Toure dakika 33', dakika ya 42' Havard Nordtveit aliyejifunga, Sergio Aguero dakika ya 51' na John stones dakika ya 84'
2,January2017 kiungo wa zamani wa klabu ya Chelsea na Timu ya Taifa ya Brazil Oscar Emboaba amejiunga na klabu ya Shanghai SIPG ya China. kiungo huyo amesajiliwa kwa ada ya pound million 52 na kulipwa 400,000 kwa wiki.
Middlesbrough imekamilisha usajili wake wa Mchezaji kutoka klabu ya
Astonvilla Rudy Gestede kwa dau la £6m amesaini mkataba wake mpaka 2020
Kipa wa Manchester united Sam Johnstone apelekwa kwa mkopo hapo Astonvilla mpaka mwisho wa msimu 2016/2017
Denis Onyango, Mlinda mlango wa Timu ya Taifa ya UGANDA amechukua Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika wa ndani. #GloCAFAwards2016
Mshambuliaji hatari wa Manchester united na timu ya zamani Fc Monaco, A.k.a "NEXT THIERRY HENRY" kwa namna anavo cheza akiwa uwanjani. Mchezaji huyu Siku za hivi karibuni ameusishwa na tetesi za kwenda kujiunga na klabu ya soka nchi Uhispania "SEVILLA".
Taarifa zinasema kuna uwezekano Mkubwa wa kijana huyu kutolewa kwa mkopo hapo "January".
OFFICIAL:
Kazi imeanza timu zimeanza kutoa ofa mbalimbali kwa ajili ya kujiimarisha kiusajili.
Hii ndiyo List ya Madili yaliyo kamilika mpaka sasa.
1: WILFRED NDINDI KWENDA LEICESTER.
Klabu ya Leicester imekamilisha usajiliwa wa Kiungo kutoka Klabu ya GENK Kiungo huyo amesaini mkataba wa miaka mitano.
2: JULLIAN DRAXLER KWENDA PSG.
Matajiri wa klabu ya Paris-Saint German, PSG. Wamemtambulisha Mchezaji wao mpya kutoka klabu ya WOLFSBURG. Mchezaji huyo amesaini mkataba wa miaka 5, Kwa ada ya €36.!
3:ALEX WITSEL KWENDA CHINA.
Klabu ya Zeint imethibitisha kuwa nyota wao "Alex Witsel" ataenda kujiunga na timu ya soka China klabu ya "Tianjin Quanjian"
4:LEONARDO PAVOLETTI KWENDA NAPOLI.
Klabu ya Napoli imenasaini ya Mchezaji "Leonardo Pavoletti" kutoka Genoa hii Leo.
5:TOMAS RINCON KWENDA JUVENTUS.
Klabu ya Juventus imemtambulisha
Kiungo wao mpya "Tomas Rincon" kutoka Katika klabu ya "Genoa". Mchezaji huyo amesaini mkataba wa miaka minne
6: PAUL CLEMENT NDIYE KOCHA MPYA WA SWANSEA.
Klabu ya Swansea City hii Leo Imemteua "Paul Clement" kuwa ndiye kocha mpya wa klabu hiyo Pia amesaini mkataba wa miaka miwili na nusu.
ONYINYE WILFRED NDINDI. Ni kiungo mpya wa Leicester city amesajaliwa toka krc GENk ya UBELGIJI. amecheza timu moja na mshambuliaji hatari Wa timu ya taifa Tanzania MBWANA SAMATTA.
NAKUPA HISTORIA FUPI YA NDINDI....
Kiungo huyu alizaliwa 16 desemba 1996 huko jijini Lagos nchini Nigeria.bado kinda kabisa. Alitumia muda wake mwingi katika kucheza soka la mitaani pamoja na watoto wenzake kabla hajaonwa na maskauti Wa klabu ya GENK.
mwaka 2015 hautasahaulika kwake kwani alifanikiwa kujiunga na klabu ya GEnk na kukabidhiwa jezi namba 25. Amecheza mechi 62 katika mashindano mbalimbali kabla hajauzwa
Amelitumikia taifa lake kuanzia soka LA vijana hadi timu ya wakubwa japo bado hawaja na namba ya kudumu kikosini Kiwango chake murua kimemshawishi kocha Claudio Ranier kutoa euro millioni 15 ili kupata huduma ya kiungo huyu maridhawa. Kwa mchezaji mweusi tena kiungo hizi ni pesa nyingi sana..
Kiungo wa Chelsea Johb Obi Mikel raia wa Nigeria atimkia klabu ya Tianjin TEDA ya China baada ya kukaa Stamford Bridge miaka 10 na kutwaa makombe 11.
Mchezaji wa timu ya taifa ya Algeria na klabu ya Leicester City, Riyad Mahrez ameshinda Tuzo ya Mchezaji Bora Afrika CAF kwa mwaka 2016.
Wachezaji 11 bora zaidi barani Afrika 2016 kwa mujibu wa CAF ndio hawa.
1. Denis Onyango (Uganda)
2. Serge Aurier ( Ivory Coast)
3. Joyce Lomalisa ( DR Congo)
4. Eric Bailly ( Ivory Coast)
5. Aymen Abdennour (Tunisia)
6. Keegan Dolly (South Africa)
7. Khama Billiat (Zimbabwe)
8. Rainford Kalaba (Zambia)
9. Pierre-Emerick Aubameyang ( Gabon)
10. Riyad Mahrez ( Algeria)
11. Sadio Mane (Senegal)
Round ya pili ya ligi kuu ya England imeanza siku hii ya leo mechi 6 katika viwanja tofauti tofauti matokeo yapo hapo chini;
Middlesbrough 0-0 Leicester city
Everton 3-0 Southampton
Manchester city 2-1 Burney
Sunderland 2-2 Liverpool
West Bromwich 3-1 Hull City
West hum Albion 0-2 Man united
Michezo ya kundi B yaanza kutimua vumbi siku hii ya leo katika kombe la mapinduzi cup huko zanzibar michezo wa kwanza kati ya Azam ashinda moja kati zidi ya zimamoto.
Mchezo uliofuata ni kati Yanga na Jamhuri. Yanga akipata ushindi wa bao 6 bila ushindi huo umewafanya wawe juu katika kundi lao kwa magoli
January 1, 2017 ligi kuu ya england iliendelea kwa michezo miwili katika viwanja viwili tofauti kati ya Watford akiwa nyumbani vicarage akipokea kichapo cha goli 4 kwa 1 zidi ya Tottenham. Ila katika uwanja wa Emirates Arsenal akiwa nyumbani akipata ushindi mnene 2-0 zidi ya crystal palece magoli yakifugwa na O.Giroud katika dakika ya 17 na dakika ya 56 iwobi akifunga goli la pili. Ila goli la kwanza la Arsenal lililofungwa na mfaransa Oliver Giroud limekua kivutio kikubwa zaidi kwa wapenzi wa soka la England na kuzungumziwa sana katika mitandao ya kijamii likifananiswa na goli la mchezaji wa mancherster united Henrick mkhitaryan alilofunga zidi ya Sunderland
Jumapili ya December 18, 2016 Ligi kuu ya England imeendelea kutimua vumbi ilipigwa big match kati ya Manchester city zidi ya Arsenal. Manchester city akiwa nyumbani katika uwanja wake wa etihad.. Dakika ya 90 zimemalizika kwa ushindi mnono kwa man city bao 2-1.
Arsenal walipata goli la kwanza dakika ya 5 kupitia mchezaji wao Theo walcott na magoli ya Manchester city yalifungwa na leroy sane dakika ya 47 na dakika ya 71 Raheem sterling akimaiza mchezo.